COSTECH YAZINDUA MWONGOZO WA UTOWAJI VIBALI VYA UTAFITI ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe, Hamza Hassan Juma amesema kuwa Kuzinduliwa kwa Mwongozo wa utowaji vibali vya utafiti pamoja na kamati za maadilizi kutasaidia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusimamia  vyema utowaji wa  vibali kwa Watafiti wanje na ndani.

Mhe, Hamza ametoa kauli hiyo wakati akizindua  mwongozo  wa Utoaji wa  vibali vya utafiti pamoja na  kamati   ya miongozo ya kamati za kusimamia maadili ya utafiti  hafla iliyofanyika katika ukumbi  wa Dkt Ali Mohamed Shen Zura.

Aidha alisema, Kuwa Serikali ya  Mapinduzi kupitia  Ofisi ya Makamu wa Pili  wa Rais   ambayo  inahusika mojakwamoja katika Utowaji wa Vibali vya Utafiti kwa kuzingatia Taratibu zilizowekwa katika miongozo hiyo na Mtafiti yoyote atakayeenda kinyume na miongozo iliyowekwa na Serikali kwa ujumla haitoshindwa kumchukulia hatua mtafiti huyo.

Awali akifungua uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu wa   Tume ya Taifa   ya Sayansi na Tekenolojia (costech) Dkt. Amos Nungu. amesema kuwa  kumekuwa na wimbi kubwa la watafiti ambao hawafuati sheria wala maadili ya Utafiti kwa Serikali, hivyo kuzinduliwa kwa  miongozo hiyo kutasaidia kuweka  utaratibu wa Utowaji wa vibali vya utafiti kwa pande zote mbili za Muungano.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Mkamu wa Pili Wa Rais Dkt. Islam Seif Salum ameeleza kuwa Serikali  imekuwa na niya thabiti ya kusimamia Sera na Kuratibu tafiti pamoja na kusimamia kamati za utowaji vibali  kwa kutoa miongozo ambayo itatoa tija kwa  Tafiti za Serikali.

Aidha aliushukuru Uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Tekenojia kwa kuanzisha chombo  hiki ambacho  kitasimamia  tafiti zilizokuwa na  kipaumble  cha Taifa.

Uzinduzi huo uliokutanisha Taasisi mbalimbali za Utafiti zilizopo Zanzibar na Taasisi nyengine kutoka Tanzania bara

.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *