SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YA ONDOSHA TOZO YA SUKURI

Waziri  wa Nchi Afisi ya Rais Fedha na Mipango  Dkt  Saada Salum Mkuya  amesema Serikali  imeondosha  tozo ya  kodi ya ongezeko ya thamani  ya 15%  kwa bidhaa ya  Sukari kwa wafanyabiashara wa jumla na  Rejareja  ili kumpunguzia gharama mwananchi katika kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Ameyasema hayo mapema leo wakati alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara mbalimbali wa Zanzibar kufuatia maombi ya wafanyabiashara juu upunguzaji kodi kwa baadhi ya bidhaa, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara Sheikh Idirisa Abdul wakal Kikwajuni.

Alisema kuwa Serikali imeamua kupunguza kodi hiyo ili kuweza kuwafanya wananachi  waweze kupata bidhaa hiyo kwa urahisi na kwa wakati ambapo, kwasasa bei ya Sukuri itakuwa  kilomoja shilingi elfu moja na miatisa kwa upande wa Unguja na Elifu Mbili kwa Upande wa Pemba.

 Awali akifungua kikao hicho Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi  Mhe: Hamza Hassan Juma alisema kuwa Serikali  imekaa na wafanyabiashara na kuwasikiliza Matakwa ya wafanyabiashara na Serikali imefikia Maamuzi ya kushusha kodi hiyo  ili kuweka mazingira mazuri ya kufanyabiashara.

Aidha alisema kuwa kumekuwepo na malalamiko ya Muda mrefu ya wafanyabiashara   juu ya kodi ya Sukari   hivyo Serikali kwa kutambua umuhimu wa wafanya biashara imeamua kuondosha kodi hiyo ili kuweza kuwasaidia wananchi wote.

Akitoa maelezo juu ya  kusamehewa  kwa tozo hizo waziri  wa biashara  na viwanda Zanziabr  Mhe: Omar Said Shabani ameeleza kuwa  tozo hiyo hatoi mwanya kwa wafanyabiashara kupandisha kodi kwa wateja   na  Serikali   haitosita   kumchukulia hatua   mfanyabiashara yoyote atakaye pandisha bei kwa bidhaa  hiyo.

Mh Omari ameongeza kusema  kuwa Wizara ya  Biashara  haitosita kumchukulia hatua mfanyabishara yoyote  ambaye ataenda kinyume na maagizo  na muongozo   wa bei elekezi uliowekwa na Serikali

Kwa upande wao wafanyabiashara wameishukuru Serikali  ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa kusikia kilio cha wafanyabiashara  na kuja na Muwafaka wa kuondosha tozo hiyo   hivyo kwa upande wao hawana budi kufuata miongozo iliyowekwa na Serikali katika  kuuza bidhaa hiyo ya Sukari  bila ya kuwaathiri wananchi.

Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe Hamza Hassan Juma akizungumza katika kikao na wafanfa Biashara leo 222/03/2022

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *