MHE HAMZA APONGEZA JITIHADA ZA WAFANYA BIASHARA

Waziri Wa Nchi Afisi Ya Makamu Wa Pili Wa Rais Mhe Hamza Hassan Juma Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea Kushirikiana na Jumuiya za wafanya biashara Wakubwa na wadogo ili  kukuza Mashirikiano  Katika Kukuza  Pato lataifa

Amesema hayo Mapema leo  tarehe 06/05/2022 Wakati Akifunga Maonesho ya Miaka hamsini 58 ya Muungano Wa Tanganyika na Zanibar   Katika Viwanja Vya Maisara, ambapo Amebainisha Kuwa  faida Mbalimbali Zimepatikana   Kwa Wafanya biashara na Serikali  Kwa Ujumla Kwa kuwa  na Mashirikiano ya Karibu   Miogoni Mwao.

Akimkaribisha Mgeni Rasim,   Katibu Mkuu Afisi ya Makmamu Wa Pili Wa Rais    Thabit Idarous Faina  Amesema Kuwa    Maonesho hayo ya Bishara  Ambayo  yalilenga Kuziweka Pamoja Taasis Za Muungano Zinazofanya Kazi zake Zanzibar  yamefanikiwa  Kwa  Kiasi Kikubwa  Kwa    Kuwanganisha Wananchi  na Taasisi hizo   za  Muungano

Akigusia Suala la Uzamini  Wamaonesho hayo  Katibu  Mkuu Faina  Ameeleza  Kuwa  Zaidi ya  Asilimia 30 ya Michango  y a Wafanya Biashara imefanikisha   Kufanyika Kwa  Maonesho hayo  na Kuwa Ofisi ya Makamu Wa Pili Wa Rais Wana Zishukuru Taasisis  Zote Zilizofanikisha  Kufanyika Kwa Maonesho hayo.

Akizungumza Kwa niaba  ya  Wafanya Biashara   na Taasisi Za Muungano Mkurugenzi Wa Mamlaka ya hali ya hewa Mohammed Ngwali  Amesema Taasisi za Muungano Zimefarijika Kupata Mualiko  Wakushiriki Maonesho  hayo na Kuziomba Mamlaka husika Kuweza Kuboresha Baadhi  ya Sehemu na ili kufanya Maonesho hayo Kuwa Makubwa Zaidi

Maonesho hayo ya Kibiashara ya Kuadhimisha Mika 58 ya Muungano  wa Tanzania ya Maanza Tangu Tarehe 22 -04 na Kufikia Kilelechake   06/04/2022.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *