BANK YA DUNIA YA RIDHISHWA NA UTEKELEZWAJI WA MIRADI YA TASAF UPANDE WA ZANZIBAR.

Katibu Mkuu Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Thabit Idarous Faina amesema  Mpango wa kunusuru kaya masikin  TASAF umefanikiwa kwa kiasikikubwa katika kuwa komboa wananchi na umsikini  katika jamii.

Akizungumza kwa maniaba ya Katibu Mkuu Afisi ya Makmu wa Pili wa Rais Mkurugenzi wa Uendeshaji na Utumishi Khamisi Haji Juma wakati akiukaribisha  ugeni na wawahisani wa maendeleo  kutoka Bank ya Dunia  Ofisini  kwake vuga  unao shughulikia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kwa Upande  Tanzania.

Ameeleza kuwa Ofisi ya Makmu wa Pili wa Rais imekuwa ikishughulikia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kwa mashirikiano  Makubwa na wananchi hivyo ameuhakikishia ugeni huo  Ofisi yake itaendelea kutoa mashirikiano na  Washirika hao wa Maendeleo.

Kwaupande wake  Mkurugenzi wa Uratibu wa Shuguli za Serikali Sijabu Sulieman Pandu ameeleza  kuwa  ugeni huo kutoka  Bank ya  Dunia umeridhishwa na utekelezaji wa Miradi  ya Maendeleo  ya TASAF inayo tekelezwa Upande wa Zanzibar hasa katika kipengele cha Uhalishaji wa fedha   kwa njia ya mtandao.

Akieleza mafanikio  ya Miradi ya TASAF  amesema  Zaidi ya wanufaika  30,632 wamenufaika  na mpango  wa kunusuru kaya Masikin na wengine tayari wamesha anza kujikimu  ambao watapatiwa malipo yao ya kujiendeleza ili kupisha kaya nyengine kufaidika na mpango huo.

Akizungumza kwa Maniaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TASAF  Makao Makuu Bw.Ladislaus Mwamanga  Mkurugenzi wa  Fedha na Miradi kutoka TASAF ameeleza Kuwa jumla  ya maeneo  186 yanatekelezwa mpango wa kunusuru kaya Maskini na kwa upande wa Zanzibar kuna maeneo mawili ya Unguja na Pemba ambapo ziara ya wadau wa maendeleo ni kuangalia  jinsi gani miradi hiyo inatekelezwa kwa  upande wa Zanzibar.

Aidha ameeleza kuwa, tangu Mwaka 2014 Serikali  ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  imekuwa ikitoa Ruzuku kwa walengwa na  hadi Sasa zaidi ya walengwa elifu kumi na Tatu wana tarajiwa kupata Fedha za Kujiendeleza  na Miradi na kuachana na fedha za  Ruzuku   ili waweze kujipatia  kipato katika jamii zao.  

Nae, Mwakilisho kutoka  Bank ya Dunia anaeshusghulikia Mfuko wa Maendeleo ya Jmii TASAF kw Upande wa Tanzania  Bwa. Michele Zini  ameeleza kufurahishwa kwake na  Utekelezaji wa Miradi hiyo ya TASAF hasakatika kipengele cha uhalishwaji wa Fedha kwa njia ya mtandao  kwa Upande wa Zanzibar  na kuihakikishia  Ofisi ya Mkamu wa Pili  wa Rais  na Serikali kwa ujumula kufanya nao  kazi kwa karibu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Kimaendeleo.

Kwa upande wao wananchi  wa kijiji cha Muungoni ambao wamepata bahati ya Kutembelewa na Ugeni huo wameuomba  Uongozi wa TASAF kutosita kuwapelekea Miradi mengine ya Kimaendeleo kamavile miradi ya Maji na Masoko ili kuweza kuondokana na Changamoto ya Maji Safi na Salama katika Maeneo yao

Ugeni huo kutoka Bank ya Dunia, Norrway,  pamoja na Sweeden amabao wanawawakilisha Wahisani wamaendeleo wamepata furusa ya Kutembelea kijiji cha Muungoni  kujionea shughuli za uhalishaji wa fedha kwa njia ya Mtandao  pamoja na kutembelea Mradi wa Ujenzi wa  njia ya Wavuvi katika maeneo hayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *