Wafanyakazi OMPR wafundwa

MKURUGENZI  Idara ya Uendeshaji  na Utumishi Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Khamis Haji Juma, amesema kutokana na mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji na uhifadhi wa kumbukumbu na nyaraka unaoenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na  technolojia, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais   imeamua kuwapatia mafunzo ya kutunza kumbukumbu kwa njia ya E-Ofisi.

Ameeleza hayo wakati akifungua mafunzo ya siku mbili yaliyowakutanisha Maofisa Utumishi, watunza kumbukumbu, wahasibu na Maofisa Tehama (IT) Ofisini kwake Vuga.

Amesema kwa mda mrefu Serikali  imekuwa  ikifanya mageuzi katika  usimamizi wa kuhifadhi Nyaraka  za Serikali  kupitia  Mradi wa huduma za umma Zanzibar ambao umedhamiria kuimarisha  utunzaji wa Masijala katika Ofisi za Umma.

Aidha, Mkurugenzi Khamis aliwataka washiriki wote kuyatumia vyema mafunzo hayo katika kuleta mataokeo mazuri yaliyo tararijiwa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu, Zanzibar Khatib  Sulieman  Khatib  amesema  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  imeziagiza  taasisi zote za serikali kuanza kutumia mfumo wa E-ofisi amabao utawasaidia watunza kumbukumbu katika ufanisi wa kazi zao.

Aidha, alieleza kuanzishwa kwa Mfumo huo kutasaidia  kurahisisha  uhifadhi wa kumbukumbu kwa haraka ndani na nje ya tasisi kufikia lengo la Serikali lililokusudiwa.

Akizungumza kwa niaba ya   washiriki wa mafunzo  hayo, Ofisa kumbukumbu kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Raisi,   Sineyu  Mabruk Jabu amewataka washiriki wamafunzo hayo kuyatumia kwa masilahi mapana ya serikali bila ya kusahau mfumo  wazamani wa kutunza kumbukumbu.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Nyaraka Zanzibar, yaliwashirikisha watumishi 40 kutoka Taasisi na Ofisi zote za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *