Majukumu

MAJUKUMU MAHSUSI YA OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS.

Katika kufikia lengo la uratibu wa shughuli za Serikali, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais imewekewa majukumu kama ifuatavyo:-

  • Kutoa huduma bora kwa Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais;
  • Kuratibu shughuli zote za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na za Muungano, ikiwemo miradi iliyo chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya SMZ;
  • Kuratibu shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
  • Kuratibu na kusimamia shughuli za utafiti kitaifa;
  • Kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala.
  • Kujenga uhimili wa jamii katika kukabiliana na maafa;
  • Kusimamia na kuratibu Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa pamoja na shughuli za kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa;
  • Kusimamia masuala ya Watu wenye Ulemavu;
  • Kusimamia shughuli za Upigaji chapa Serikalini;
  • Kuratibu shughuli za Tume ya Uchaguzi;
  • Kuratibu shughuli za Baraza la Wawakilishi;
  • Kuratibu shuguli za Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya Zanzibar pamoja; na
  • Kuratibu shughuli za Tume ya UKIMWI ya Zanzibar.